Jinsi ya kuwatumia wasomaji habari unazoandika

By ndesanjo

Yapo mambo kadhaa ambayo mwenye blogu anaweza kufanya ili kusaidia wasomaji kwa kurahisisha upatikanaji wa habari unazoandika. Kati ya mambo hayo ni huduma inayowezesha wasomaji kutumiwa mambo unayoandika kwa barua pepe. Msomaji anachotakiwa kufanya ni kuweka anuani yake kwenye fomu utakayoweka kwenye blogu yako kisha atatumiwa habari mpya kila unapoandika. Huduma nitakazokupa ni za bure (ingawa zipo pia za kulipia). Kama ungependa kuwapa wasomaji wako huduma hii, unaweza kutumia huduma kati ya hizi nitakazoorodhesha hapo chini. Ukiwa na tatizo ya jinsi ya kutumia huduma hizo au kuziweka kwenye blogu yako unaweza kuniandikia: ughaibuni@yahoo.com (HAKIKISHA KICHWA CHA WARAKA WAKO KINASEMA: MWONGOZO WA BLOGU)(LA SIVYO BARUA YAKO INAWEZA IKACHUKUA MUDA MREFU KUSOMWA).

Huduma ni hizi:

1. FEEDBLITZ: http://www.feedblitz.com/

2. SQUEET: http://www.squeet.com/

3. YUTTER: http://www.yutter.com/

4. AWEBER: http://www.buniek.com/

5. ZOOKODA: http://www.zookoda.com/

3 Responses to “Jinsi ya kuwatumia wasomaji habari unazoandika”

  1. Jikomboe » Huduma za kutumia wasomaji habari zako Says:

    [...] Kuanzia sasa kutakuwa na maudhui yaitwayo “zana” ambayo kazi yake ni kutoa taarifa za zana mbalimbali ambazo zinaweza kuwa muhimu kwa wanablogu au kwa mtu yeyote anayefuatilia mabadiliko ya zana za habari na mawasiliano.   Kwa mfano, kuna huduma mbalimbali ambazo unaweza kutumia ili kuwezesha wasomaji wako wawe wanapokea habari unazoandika kwa njia ya barua pepe.  Bonyeza hapa uzione huduma hizo.   [...]

  2. birdhil Says:

    Great job guys… Thank for you work…

  3. segisekure Says:

    tunakushkulu sana,nadhani sio haki mtu kunyamanza bilakukupa sifa zako. kusemakweli uko juu sanahapa tanzania kwa wote wana blog nawaomba wakubali hilo. sasanaomba nikuulize je.ukiwa umefunguwa blog yako unaweza kuipata wapi ili uone kamaimeshakuwa tayari? ni hilo ndugu machanakutakia kazi njema.

Leave a Reply